Mo Dewji: Hakuna mtu yeyote aliye mkubwa kuliko klabu ya Simba



Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Klabu ya Simba, modewji amesema hakuna mtu yeyote aliye mkubwa kuliko klabu ya Simba.

“Hakuna mtu mkubwa kuliko Simba, hata mimi mwenyewe Mohammed Dewji sio mkubwa kuliko Simba,”.Mo Dewji

Mo Dewji ameendelea kusema kuwa amekuwa akiumizwa na madai kuwa hana bilioni 20 alizoahidi kuwekeza Simba Sc, na leo amezitoa ili mjadala huo uishe.

"Leo naweka hiyo Bilioni 20 ya hisa asilimia 49 mbele ya mdhamini wa klabu na mwenyekiti wa klabu."- Mo Dewji.

Post a Comment

0 Comments