Shirika la Umoja wa Mataifa la ukaguzi wa nyuklia IAEA limefikia makubaliano na Iran kuhusiana na kuvifanyia marekebisho vifaa vya ukaguzi kwa ajili ya kuendesha shughuli zake.
Suala hilo lilikuwa ni la
dharura na suluhisho hilo lililopatikana linaleta matumaini ya
mazungumzo mapya ya mkataba wa nyuklia na mataifa ya Magharibi.
Mkuu wa
shirika hilo Rafael Grossi alipata makubaliano hayo katika ziara ya
dakika ya mwisho ya Tehran kabla kufanya mkutano na magavana wa IAEA
wiki hii ambapo nchi za Magharibi zenye nguvu zilikuwa zinatishia
kutafuta suluhisho la kuikosoa Iran kwa kulizuia shirika hilo kutekeleza
majukumu yake.
Suluhisho hilo lilikuwa na hatari ya kuzidisha mvutano
baina ya Iran na Marekani ambao ungekuwa kikwazo kwa mazungumzo ya
kuufufua mkataba wa nyuklia wa mwaka 2015 kati ya Iran na Marekani.
0 Comments