Na Amiri Kilagalila,Njombe.
Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe (CCM) ambaye ni diwani wa kata ya Njombe mjini Bwana. Romanus Mayemba (Starmius) amefariki Dunia jana Oktoba 23/2021 katika hospital ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mayemba alikwenda hospitali ya Benjamini Mkapa siku ya Ijumaa kwa ajili ya matibabu.
Aidha mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa na kurejea mjini Njombe katika mtaa wa Msete hapo kesho Octoba 25/2021
0 Comments