Tanzia: Mwenyekiti wa halmashauri ya mji Njombe afariki Dunia


Na Amiri Kilagalila,Njombe.

Mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe (CCM) ambaye ni diwani wa kata ya Njombe mjini Bwana. Romanus Mayemba (Starmius) amefariki Dunia jana Oktoba 23/2021 katika hospital ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.

Mayemba alikwenda hospitali ya Benjamini Mkapa siku ya Ijumaa kwa ajili ya matibabu.

Aidha mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa na kurejea  mjini Njombe katika mtaa wa Msete hapo kesho Octoba 25/2021

 

Post a Comment

0 Comments