Miguu yao imewekewa bima ya mamilioni ya dola

 


Miguu ya mwanamitindo mwenye uraia wa Marekani na Ujerumani Heidi Klum imewekewa kwenye bima ya mamilioni ya dola, ili iwe na muonekano bora wakati wote.

Mwanamitindo huyu mwenye umri wa miaka 48 alifichua kwa mara ya kwanza mwaka 2011 kwamba miguu yake imewekewa bima ya dola milioni 2.2.

Garama ya miguu ya Heidi hivi karibuni imekuwa mada ya kujadiliwa naada ya kushiriki kwenye mazungumzo na kipindi cha Televisheni cha cha The Ellen DeGeneres wiki hii

Katika mazungumzo hayo alisema mguu wake mmoja ni ‘’ghali kuliko mwingine’’

Aliliambia jarida la People Magazine mwaka 2017 kwamba mguu wake mmoja unagarimiwa dola milioni 1.2 na mwingine dola milionina ndio maana hadi sasa watu wanamtamani akiwa na miaka 40 na ushee.

"Kila mara nafurahia kuvaa sketi fupi sana( mimi skirt) ili kuoyesha miguu yang una bado ninaipenda ,"

Watu wengine watano maarufu walioweka bimaya juu ya miguu yao

Taylor Swift

Muimbaji wa muziki wa pop amekuwa akivaa mavazi ya kuonyesha miguu yake baada ya kuweka bima ya dola milioni 40 kwa ajili ya miguu yake tu(milioni $20 kwa kila mguu), alisema hayo kabla ya kuanza safari yake ya kimuziki aliyoiita 1984 Tour mwaka 2015.

Mariah Carey



Miguu ya Mariah Carey imewekewa bima ya dola bilioni 1.

Pia aliweka a bima ya sauti yake ya dola milioni 35, kwa ajili yatamasha la muziki la Sweet Sweet Fantasy Tour mwaka 2011.

Cristiano Ronaldo


Miguu ya mchezaji wa kimataifa wa soka wa Ureno na mshambuliaji wa Man United Striker, Cristiano Ronaldo pia hayuko nyuma katika kuiweka miguu yake katika bima ya bei kali.

Real Madrid iliweka bima ya miguu yake ili kuizuwia kupata majeraha alipojiunga na klabu hiyo 2009. Waliiwekea bima miguu ya Ronaldo ya dola milioni 144.

Lionel Messi


Mchezaji wa kimataifa wa Argentina wa soka, Lionel Messi analipiwa bima ghali zaidi kuliko wote kwa ajili ya miguu yake. Mguu wa Messi wa kushoto umewekewa bima ya dola milioni 900.

Tina Turner


Ni maarufu sawa na miguu yake pamoja na uwepo wake kwenye jukwaa. Miguu ya huyo Mmarekani huyo Mzaliwa wa Uswiss imewekewa bima ya dola milioni 3.2


Post a Comment

0 Comments