Sudan yamuita balozi wake Adis Ababa kupinga kuuawa kwa wanajeshi wake Ethiopia

Sudan yamuita balozi wake mjini Adis Ababa kwa ajili ya mazungumzo katika hatua ya kupinga madai ya kuuawa kwa wanajeshi saba na jeshi la Ethiopia. Khartoum imemuita pia balozi wake nchiniSudan kuelezea hali iliyozingira mauaji ya wanajeshi kwenye mpaka unaozozaniwa baina ya nchi hizo.

Jumapili jeshi la Sudanlilisema kwamba wanajeshi waliouawa walikuwa mateka lakini waliuawa na miili yao ilionyeshwa mbele ya umma. Imesema kutakuwa na jibu linalofaa kwa mauaji hayo lakini hakuelezea ni hatua gani hasa ambazo serikali ya Khartoum itazichukua. Ethiopia imekanusha mauaji hayo .

Hali ya wasi wasi imeendelea kutanda baina ya Ethiopia na Sudan juu ya eneo la kilimo lenye rutuba lililopo baina ya mpaka hizo mbili. Makabiliano baina ya vikosi vya Ethiopia na Sudan yamekuwa ya kawaida kwa miongo , lakini yameongezeka katika muda wa mwaka uliopita. Mkataba baina ya nchi hizo katika mwaka 2008 umeshindwa kumaliza mzozo. Ethiopia na Sudan pia zimekwama katika mzozo juu ya ujenzi wa bwawa kubwa la umeme kwenye Mto Nile.

 

Post a Comment

0 Comments