https://monetag.com/?ref_id=TTIb Tetesi za Soka Ulaya leo 25.06.2022 | Muungwana BLOG

Tetesi za Soka Ulaya leo 25.06.2022

Arsenal wamefikia makubaliano ya kumnunua mshambuliaji wa Manchester City na Brazil Gabriel Jesus, huku The Gunners wakipanga kulipa pauni milioni 45 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Fabrizio Romano)


Kiungo wa kati wa Uholanzi Georginio Wijnaldum ataruhusiwa kuondoka Paris St-Germain msimu huu wa joto. Leicester City wanamtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, wakati Everton, Wolves na West Ham pia wanafuatilia kwa karibu hali hiyo. (90min)


Meneja wa Chelsea Thomas Tuchel ameahidiwa kusajiliwa kama wachezaji sita msimu huu na wamiliki wapya wa klabu hiyo. (Telegraph - subscription required)


Mkurugenzi wa Bayern Munich Hasan Salihamidzic anasema hakuna ukweli katika uvumi kwamba klabu hiyo ya Bundesliga inataka kumsajili mshambuliaji wa Manchester United na Ureno Cristiano Ronaldo, 37. (Sky Germany - in German)


Leeds na winga wa Brazil Raphinha, 25, amekataa ofa kutoka kwa vilabu vingine vya Premier League kwa sababu anataka kujiunga na Barcelona. (Sport - in Spanish)


Chelsea itasikiliza ofa kwa mlinda mlango wa Uhispania Kepa Arrizabalaga baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kuiambia Marca kwamba ‘’lengo lake wazi ni kucheza.’’ (Mirror)


Manchester United na Ralf Rangnick walikubali kukata uhusiano mwishoni mwa msimu uliopita kwa kiasi fulani kwa sababu ya meneja mpya Erik ten Hag kusita kufanya kazi na Mjerumani huyo katika jukumu lake la ushauri lililopendekezwa. (ESPN)


Barcelona wanatumai Tottenham inaweza kumshawishi mlinzi wa kati wa Ufaransa Clement Lenglet, 27, kuhamia Ligi ya Premia ili timu hiyo ya La Liga ianze kuwaondoa wachezaji wakati wa msimu. (ESPN)


Tottenham na Middlesbrough bado hawajaafikiana kuhusu ada ya uhamisho wa beki wa kulia wa timu ya taifa ya Uingereza chini ya umri wa miaka 21 Djed Spence, kwa kuwa timu hiyo inayoshiriki Ligi ya Mabingwa inataka takriban pauni milioni 15 pamoja na nyongeza kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21. (Sun)


Winga wa Brazil Anthony, 22 - ambaye ana nia ya kuungana na meneja wa zamani Erik ten Hag katika Manchester United - alikosekana wakati Ajax iliporejelea mazoezi ya kujiandaa na msimu Ijumaa. (Mirror)

 

Post a Comment

0 Comments