Museveni akanusha kwamba anamtayarisha mwanawe kuchukua wadhifa wa urais

 


Mwanahabari wa BBC Alan Kasujja amepata fursa ya kuzungumza na Rais wa Uganda Yoweri Museveni.


Kabla ya kuanza mazungumzo yao, walikuwa na muda mfupi wa kutaniana.


Akizungumza naye kwa kipindi cha BBC cha Africa Daily, alimuuliza kama Uganda inakaribia Urusi na Uchina, na akasema kuwa nchi hizi hazikuwa wakoloni au wafanyabiashara wa utumwa zamani.


Anasema siku zote wameingia barani kama marafiki.


Kasujja alipohoji jukumu la upinzani nchini Uganda, alimrudisha nyuma hadi mwaka 1789 - mapinduzi ya Ufaransa na mageuzi ya demokrasia huko Uropa.


Uganda iko kwenye njia tofauti, Rais Museveni anasema.


Anapoelezea msimamo wake kuhusu vita vya Ukraine, analinganisha uwepo wa Nato katika Ulaya ya Mashariki na mzozo wa makombora wa Cuba mwaka 1962.


Alan akaanza kushangaa jinsi majibu hayo yanahusiana na idadi ya vijana ya Uganda inayozidi kuongezeka.


Zaidi ya 77% ya watu hapa wako chini ya umri wa miaka 30.


Alan: Kutokana na mazungumzo ambayo nimekuwa nayo wiki iliyopita, yanalenga mahitaji yao ya haraka - iwe wanaweza kumudu kupanda kwa gharama ya maziwa ya watoto, gharama za matibabu na kama kutafuta kazi hapa au kusafiri ng’ambo.


Rais haoni tofauti hii.


Ananiambia: “Unachoita historia Bw Kasujja, mimi naita mambo ya sasa.”


Lakini akiangalia siku zijazo, inaonekana yuko tayari kujihusisha na wazo la mabadiliko.


Nilimuuliza swali lililoulizwa wakati wa mjadala niliofanya na vijana wasomi katika mji mkuu - ikiwa wanaulizwa kukaza mikanda yao, kwa nini wanasiasa hawawezi kuzuia matumizi yao ya magari makubwa, madereva na safari za watendaji?


Bw Museveni anasema hilo swali ni sahihi na haki kuulizwa.


Ninapouliza kwa nini hajatoa mwongozo wa athari hiyo, anasema lingekuwa wazo zuri.


Katika mada ya kupanda kwa bei ya mafuta, anasema nchi inapaswa kuwa katika mpito kwa magari ya umeme na treni.


Ingepunguza bei ya bidhaa kwa kila mtu, anaamini.


Lakini vipi kuhusu hatma yake ya baadaye?


Alan: Ninashirikishana naye angalizo kwamba viongozi wengi mashuhuri wa Uganda - Waziri Mkuu, Makamu wa Rais, Spika wa Bunge - wanatoka kizazi kipya katika miaka yao ya 40 na ya awali ya 50.


Ninauliza kama tunashuhudia mwanzo wa mpito wa madaraka.


“Ndio,” ananiambia, “watu wanakuja. .”


Anakanusha kuwa anamtayarisha mwanawe - Luteni Jenerali Muhoozi Kainerugaba, kamanda wa vikosi vya ardhini vya Uganda - kuchukua wadhifa wa urais.


Lakini anasisitiza kwamba kizazi kijacho cha viongozi kinapaswa kutoka katika chama chake, National Resistance Movement.


Kwa hiyo, baada ya miaka 35 kuongoza nchi, yuko tayari kutumia muda zaidi shambani na ng’ombe wake – pengine kustaafu?


“Kuna raha sana huko.


Ningeweza kwenda wakati wowote” anasema “sihitaji kazi”.


Lakini lazima nimkumbushe…aliniambia vivyo hivyo tulipozungumza mnamo mwaka 2013.

Post a Comment

0 Comments