https://monetag.com/?ref_id=TTIb Kenya kuzindua kampeni ya chanjo surua huku ikikabiliwa na mlipuko | Muungwana BLOG

Kenya kuzindua kampeni ya chanjo surua huku ikikabiliwa na mlipuko

 


Wizara ya afya nchini Kenya itazindua kampeni ya wiki mbili dhidi ya ugonjwa surau ikiwalenga watoto milioni 1.2 m wenye umri wa miezi tisa handi miaka mitano.


Hii inafuatia mlipuko wa ujongwa huo kuzikumba kaunti 7 ambapo 90% ya watoto wenye chini ya umri wa miaka mitano walikosa dozi mbili za chanjo hiyo.


Ukame unaoendelea katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo umeifanya shughuli ya utoaji wa chanjo hiyo kuwa ngumu kwa wahudumu wa afya kutoa chanjo hiyo muhimu kwa maisha ya watoto, kutokana na watu kuhama kutoka sehemu moja kuelekea sehemu nyinginekusaka chakula na maji.


Wizara ya afya bado haijafichua ni visa au vifo vingapi viliripotiwa , lakini inawataka wazazi na walezi kuhakikisha kuwa watoto wanapata chanjo ili kudhibiti mlipuko wa maradhi hayo.


Surua ni ugonjwa unaoambukiza haraka na husababisha mgonjwa kuwa vipimo vya juu vya joto na upele. Utoaji wa chanjo umepungua kote duniani tangu lilipotokea janga la Covid – 19.


Kampeni inatarajiwa kuanza Ijumaa na kumalizika tarehe 18 Disemba.

Post a Comment

0 Comments