Shirika la Trump lapatikana na hatia ya uhalifu unaohusu kodi baada ya kesi ya New York

 

Kampuni ya makazi ya rais wa zamani wa Marekani Donald Trump imepatikana na hatia ya uhalifu wa kodi.


Shirika la Trump limepatikana na hatia kwa makosa yote Jumanne baada ya jopo la mahakama kufanyia uchunguzi kesi yake kwa siku mbili na kutoa tathmini yake mjini New York.


Biashara hiyo ya makazi inahusishwa na rais huyo wa zamani wa marekani, iwe Bw Trump au watu wa familia yake hakuna aliyekuwepo mahakamani binafsi katika kesi hiyo.


Akiapa kukata rufaa juu ya kesi hiyo, Bw Trump alisema kuwa ame "katishwa tamaa" na akaielezea tena kesi hiyo kama ya "hila".


Kampuni hiyo ilipatikana a hatia ya kuwatajirisha wakuu wake kwa faida ambazo hazikusajiriwakwa zaidi ya muongo.


Vitu ambavyo havikulipiwa kodi ni pamoja na magari ya kifahari na ada za shule za kibinafsi, ambapo waendesha mashitaka walisema, walidanganya kulipwa mishahara ya chini na hivyo kupunguza kiwango cha kodi ambayo biashara hiyo ilitakiwa kulipa.


Kampuni hiyo inatarajiwa kukabiliwa na faini ya karibu dola milioni 1.6(£1.3m) na pia huenda ikakabiliwa na ugumu katika upataji wa mikopo na fedha siku zijazo.



Post a Comment

0 Comments