Kenya yakanusha uchunguzi wa ukwepaji kodi kwa familia za marais wa zamani


Waziri Mkuu wa Kenya, Musalia Mudavadi, amekanusha ripoti kwamba familia za marais wa zamani Jomo Kenyatta na Daniel Moi zililengwa kwa madai ya kukwepa kulipa kodi. Bw Mudavadi alisema Rais William Ruto hakutaja majina yoyote katika harakati zake za kufuata ushuru, na anadai ripoti hizo ni miongozo iliyotolewa na vyombo vya habari.


Hata hivyo anasisitiza kuwa kila mtu lazima alipe ushuru ili kusaidia serikali kuendesha shughuli zake.


Kauli hii Inafuatia baada ya kusambazwa kwa video kwenye mitandao ya kijamii ya Mke wa Rais wa zamani Ngina Kenyatta, ambapo alisema hadharani familia yake ilikuwa imelipa kodi zote zinazodaiwa.


Aliongeza kuwa yuko tayari kuchunguzwa kwa kukwepa kulipa kodi na kwamba yuko tayari kulipa malimbikizo yoyote iwapo madai ya kutolipwa kodi yanaweza kuthibitishwa.

Post a Comment

0 Comments