Morris aagwa rasmi Taifa Stars

 


Beki wa Azam FC na timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Aggrey Morris (36) leo ameagwa rasm kuichezea Taifa Stars baada ya kuomba kustaafu timu ya taifa.

Morris ameagwa leo kwa kucheza mchezo wake wa mwisho Taifa Stars wa kirafiki dhidi ya Congo DR.

Hata hivyo Morris alikabidhiwa mfano wa hundi ya Tsh milioni 5 na jezi iliyosainiwa na wachezaji wote wa Taifa Stars kama sehemu ya kumuaga kwa utumishi wake wa muda wote Taifa Stars.

Post a Comment

0 Comments