https://monetag.com/?ref_id=TTIb Serikali ya Afghanistan kuendeleza mazungumzo na Taliban kwa ajili ya kusitisha mapigano | Muungwana BLOG

Serikali ya Afghanistan kuendeleza mazungumzo na Taliban kwa ajili ya kusitisha mapigano


Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Upatanisho wa Kitaifa wa Afghanistan Abdullah Abdullah, alisema kwamba wanataka kutekelezwa kwa mazungumzo ya makubaliano yanayoendelea na Taliban katika mji mkuu wa Qatar Doha kwa ajili ya kusitisha mapigano.

Katika hotuba yake aliyoitoa kwenye hafla aliyohudhuria katika mji mkuu wa Kabul, Abdullah alisema kuwa timu ya wajumbe wa Afghanistan inaendeleza mazungumzo na Taliban huko Doha kwa mamlaka kamili.

Akibainisha kuwa kipaumbele cha timu ya wajumbe wa Afghanistan ni kuhakikisha kusitisha mapigano, Abdullah alisema,

"Tunataka kukomesha migogoro na kusitisha mapigano kupitia mazungumzo yanayoendelea Doha kati ya pande zote za Afghanistan."

Abdullah pia alisisitiza uhitaji wa maoni ya kikanda na kimataifa ili kufanikisha makubaliano ya amani nchini Afghanistan.

Mazungumzo ya awamu ya pili kati ya Afghanistan na Taliban yalianzishwa tena tarehe 6 Januari, baada ya kusitishwa kwa idhini ya pande zote husika mnamo Desemba 14.


Post a Comment

0 Comments