https://monetag.com/?ref_id=TTIb Tumeshampendekeza Mrithi Wa Maalim Seif | Muungwana BLOG

Tumeshampendekeza Mrithi Wa Maalim Seif


Sehemu ya hotuba ya kiongozi wa chama Cha ACT Wazalendo Ndg, Zitto Kabwe kwenye khitima ya kumuombea Maalim Seif iliyofanyika Dar-es-salaam.


"Tayari tumeshapendekeza jina kwa rais wa Zanzibar la mtu Ambaye atarithi Majukumu Ambayo Maalim Seif alikuwa anafanya.


Bahati nzuri Maalim alikuwa ni kiongozi bora na alijua kuna siku mwenyezi mungu atamchukua kwasababu sisi sote lazima turejee kwa Mwenyezi mungu kama kama tulivyoambiwa na mafunzo ya dini zetu.


Kwa hiyo aliacha  Ametupa maelekezo ya nini kitokee endapo atatangulia Mbele ya Haki.


Namshukuru mwenyezi mungu kwamba viongozi wa chama wamsfuata yale Maelekezo yake kwa namna ambayo kiongozi wetu alituelekeza. Sasa umebaki wajibu wa Rais wa zanzibar kuyatekeleza hayo.


Sisi tunaamini kabisa kuwa huyo Ambaye amependekezwa ataweza kusimamia Maridhiano na haki za wazanzibar kama ambavyo Maalim seif alisimamia.


Tunawaomba muendelee kutuombea duwa ili tusitoke kwenye mstari, tuendelee kupigania demokrasia, haki na kuhakikisha kuwa nchi yetu inaendelea kuwa ya Amani ya Amani iliniweze kupata Maendeleo ya Watu"

Post a Comment

0 Comments