Nandy avunja ukimya, afunguka ishu ya Ukimwi

 


Msanii Nandy 'The African Princes' amevunja ukimya kwa kutaka watu waache kuumuliza kuhusu kudaiwa kuwa na ugonjwa wa Ukimwi kwa sababu itawafanya wale wanaoumwa kweli ugonjwa huo wajione sio binaadam wa kawaida.


Akitoa taarifa hiyo kwenye 'Insta Story' yake ya mtandao wa Instagram Nandy ameandika kuwa 


"Swali la Ukimwi pia muache kuniuliza otherwise unataka nikupunguzie kidogo na tuheshimiane, mnafanya hata wale wanaoumwa kweli wajione sio binaadam wa kawaida hofu ya Mungu itawale" amesema Nandy


Aidha Nandy ametoa taarifa nyingine ambayo inadhibitisha kuachana na Billnass ambapo anasema hataki kuulizwa kuhusu mahusiano tena na wampe muda wa miaka mitana tena.

Post a Comment

0 Comments