Taliban yatuhumiwa kwa mauaji ya waandishi wa habari wa kike

 


Serikali ya Afghanistan iliishutumu Taliban kwa vifo vya wafanyikazi 3 wa kike wa kituo cha kibinafsi cha runinga vilivyotokea katika mkoa wa Nangarhar hapo jana.


Rais wa Afghanistan Ashraf Ghani alisema katika taarifa yake kwamba Taliban wanajaribu kuunda mazingira ya ukatili kwa kufanya mashambulizi kama haya na kuzima sauti ambazo zinapazwa kutetea jamhuri.


Maafisa wa polisi wa Nangarhar pia walitangaza kuwa watu 3 ambao walifanya shambulizi hilo walikamatwa na baada ya kuhojiwa, walifikia hitimisho kwamba shambulizi hilo lilitekelezwa na Taliban.


Msemaji wa Taliban Zabihullah Mujahid alidai kwamba hakuwa na uhusiano wowote na shambulizi hilo.


Katika taarifa iliyotolewa na shirika la kigaidi la DAESH, ilidaiwa kuwa wao ndio waliohusika na mauaji ya wafanyikazi watatu wa kike wa shirika la habari linalounga mkono serikali ya Afghanistan.


Mnamo Desemba 2020, mwandishi wa habari wa kike Malalai Meywand, ambaye alifanya kazi kwenye idhaa hiyo hiyo ya runinga, pia alikufa katika shambulizi la silaha.

Post a Comment

0 Comments