Arsenal, Chelsea, Liverpool, Manchester City, Manchester United na Tottenham zakubali kujiunga na Ligi Kuu ya Ulaya


Arsenal, Chelsea, Liverpool, Manchester City, Manchester United na Tottenham ni miongoni mwa vilabu 12 ambavyo vimekubali kujiunga na Ligi Kuu ya Ulaya (ESL).

Katika hatua ambayo huenda ikayumbisha soka huko Uropa, vilabu hivyo vya Ligi ya premia vitajiunga na AC Milan, Atletico Madrid, Barcelona, Inter Milan, Juventus na Real Madrid katika kuunda ligi mpya ya bara ulaya .

ESL ilisema vilabu waanzilishi vilikubaliana kuanzisha "mashindano mapya ya katikati ya wiki" na timu zinazoendelea "kushindana katika ligi zao za kitaifa".

Inasema msimu wa uzinduzi "unakusudiwa kuanza mapema iwezekanavyo" na "ilitarajia kwamba vilabu vingine vitatu vitajiunga na" ligi hiyo .

ESL inasema pia ina mpango wa kuzindua mashindano ya wanawake haraka iwezekanavyo baada ya mashindano ya wanaume kuanza.

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson, Uefa na Ligi Kuu Uingereza walilaani hatua ya kuzindua Ligi Kuu ya Ulaya wakati habari hizo zilipotolewa siku ya Jumapili.

Shirikisho la soka duniani Fifa limesema hapo awali halitatambua mashindano kama hayo na wachezaji wowote wanaohusika katika mechi hizo wanaweza kunyimwa nafasi ya kucheza kwenye Kombe la Dunia.

Uefa, shirikisho linalosimamia soka Ulaya, lilikariri onyo hiyo siku ya Jumapili wakati liliposema wachezaji wanaohusika watapigwa marufuku kutoka kwa mashindano mengine yote katika ngazi ya nyumbani, Ulaya au ulimwengu na wanaweza kuzuiwa kuwakilisha timu zao za kitaifa.

Baada ya Ligi hiyo kuu Kuu ya Ulaya kutangazwa, Fifa ilielezea "kutokubali" mashindano hayo yaliyopendekezwa na kutoa wito kwa "pande zote zinazohusika katika majadiliano kushiriki mazungumzo ya utulivu, yenye kujenga na yenye faida kwa mchezo wa soka ".

Katika taarifa, ESL ilisema: "Kwa kuendelea, vilabu vya waanzilishi vinatarajia kufanya majadiliano na Uefa na Fifa kufanya kazi pamoja kwa kushirikiana kutoa matokeo bora kwa ligi mpya na kwa soka kwa ujumla."

Post a Comment

0 Comments