Azam yabanwa mbavu na Dodoma


Klabu ya Azam FC imetoshana nguvu na Dododma jiji FC kwa kutoka sare ya mabao 2-2, katika mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara uliochezwa katika dimba la Jamuhuri Dododma.

Azam FC ndio walikwa wa kwanza kufunga bao kupitia kwa Prince Dube dakika ya pili ya mchezo, lakini baadae kipindi cha pili dakika ya 71 Seif Karihe akaisawazishia Dodoma Jijiji na dakika 6 baadae Anuary Jabir akafunga tena bao la pili na kuipa uongozi Dodoma mpaka dakika ya 90 ambapo Azam FC wakasawazisha kupitia kwa Obrey Chirwa.

Kwa ushindi huu Azam wanasalia nafasi ya tatu wakiwa na alama 51, wakatia Dodoma wanafikisha alama 38 wakiwa nafasi ya 6 kwenye msimamo wa ligi.

ukiachana na mchezo huo, Mchezo wa mapema leo ulichezwa Saa 8:00 mchana ambapo Ihefu FC walikuwa wenyeji wa Tanzania Prisons, na wenyeji wakafanikiwa kuondoka na alama zote tatu baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0, bao la pekee katika mchezo huo limefungwa na Raphael Daud dakika ya 6.

Ihefu imepanda kwa nafasi moja kutoka ya 17 hadi 16 wakifikisha alama 27, na Tanznaia Prisons wameshuka kwenye msimamo kutoka nafasi ya 8 mpaka ya 9 wakisalia na alama 34.

Post a Comment

0 Comments