Breaking News: Nyalandu atangaza kurejea CCM

 


Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu leo Ijumaa Aprili 30, 2021 ametangaza kurejea CCM katika mkutano mkuu maalum wa chama hicho tawala mkoani Dodoma. Nyalandu alijitoa CCM Oktoba 30, 2017 akiwa mbunge wa Singida Kaskazini na baadaye kujiunga na Chadema ambako alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Kati. Pia alijitosa katika kura ya maoni ndani ya Chadema mwaka 2020 kuwania kuteuliwa kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, 2020 kwa tiketi ya chama hicho.

Post a Comment

0 Comments