Fahamu kuhusu ugonjwa wa Polio kiundani zaidi

Polio ni ugonjwa wa kuambukiza usababishwao na virusi, huathiri neva na kusababisha ulemavu.

Kutokana na taarifa za shirika la afya duniani:
Polio huathiri zaidi watoto wa umri wa chini ya miaka mitano
Ulemavu hutokea kwa mmoja kati ya maambukizi 200
Mpaka 2013 ni nchi tatu ambazo bado kuna mlipuko wa ugonjwa huu wa kupooza Afghanistan, Pakistan na Nigeria. Ila kutokana na Taarifa kutoka wizara ya afya ya Tanzania ilipokea taarifa kutoka shirika la afya duniani kuwa kuna mlipuko katika nji jirani ya Kenya, wilaya ya Fafi.

Je ni zipi dalili za ugonjwa huu?
Dalili hizi hudumu kwa kati ya siku 1 hadi 10
Homa
Maumivu ya kichwa
Kutapika
Uchovu
Maumivu ya shingo
Maumivu ya mgongo
Maumivu ya mikono na miguu
Misuli kukakamaa

Je ni matatizo gani mtu huweza kupata baada ya maambukizi haya?
Kupooza misuli
Ulemavu wa miguu

Vipimo:
Virusi vya polio huweza kuonekana katika makohozi, kinyesi na maji maji ya uti wa mgongo.

Matibabu
Hamna matibabu ya maambukizi haya, kwahiyo ni tiba ya dalili ambayo hutolewa:
Kupumzika
Dawa za kutuliza maumivu na kushusha homa
Antibiotiki kuzuia maambukizi nyemelezi
Mazoezi kiasi kwaajili ya kuzuia kukakamaa
Na kula chakula bora

Kinga
Ni chanjo ya Polio ambayo hutolewa pamoja na chanjo nyingine kwa watoto baada tu ya kuzaliwa, na kurudiwa tena katika wiki ya nne, ya nane na mwisho ya kumi na mbili.

Post a Comment

0 Comments