Kenya kufunga kambi za Kakuma, Dadaab kufikia Juni 2022


Kenya imethibitisha kuwasiliana rasmi na Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR na kutaarifu kuwa itafunga kambi za wakimbizi ya Dadaab na Kakuma ifikapo Juni 30, 2022.

Waziri wa mambo ya nje wa nchini Kenya bwana Fred Matiangí ametangaza hayo baada ya kufanya mkutano na Filippo Grandi, mjumbe wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia wakimbizi.

Dkt. Matiangí amesema kuwa timu ya maafisa wa serikali ya Kenya na Shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa watafuatilia mchakato huo uliopangiwa kuanza Mei, 5, 2022.

Mchakato wa sasa hivi unajumuisha kurejea katika nchi zao kwa hiari au kutoa kibali cha kufanyakazi au cha makazi bila malipo kwa wakimbizi kutoka jamii ya Afrika Mashariki.

Wakati huo huo, Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limefurahishwa na mpango wa kupitiwa tena kwa mpango wa kufunga kambi hizo za wakimbizi.

‘’Sio kambi za kudumu za wakimbizi au kufungwa kwa haraka kwa kambi hizo au kukiuka kanuni ya kimataifa inayokataza nchi inayopokea wakimbizi kuwarejesha nchini mwao ambako wanaweza kuwa katika hatari ni suluhisho ya hili’’, UN imesema.

Katika taarifa iliyotolewa na shirika hilo, imesema kuwa inaamini serikali ya Kenya na shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa katika kubaini machaguo mengine ya kuwahifadhi au kurejea kwa hiari kwa wanaotaka kwa namna heshima.

Mnamo mwezi Machi, serikali ya Kenya ilikuwa imeipatia UN makataa ya mwisho ya kutafuta njia kwasababu inataka kufunga kambi hizo mbili ambazo ni makazi kwa wakimbizi 400,000.

Muda mfupi baadae, Shirika la Amnesty International likajibu kwa kusema kuwa hatua ya kufungwa kwa kambi za Dadaab na Kakuma bila mpangilio unaoheshimu haki za wakimbizi, kutasababisha janga la kibinadamu wakati tayari dunia inakumbana na janga la virusi vya corona.

Kenya imekuwa ikitoa makazi kwa wakambizi kwa zaidi ya miaka 30 na sasa hivi serikali inasema uwezo wake kuendelea kuwatunza hata kwa kuzingatia viwango vya chini kabisa vya kibinadamu vinavyokubalika imekuwa changamoto kwa nchi hiyo kuvifikia.

Katibu Mku nchini Kenya Karanja Kibicho, aliongeza kuwa uamuzi wake wa kufunga kambi za Dadaab na Kakuma kufikia Juni 30, 2022 ‘ni kwa maslahi ya raia wa nchi yake’.



Post a Comment

0 Comments