Manowari ya Indonesia yapoteza mawasiliano


Manowari ya KRI Nanggala-402 inayomilikiwa na kikosi cha Indonesia, na ambayo ina wafanyikazi 53, iliripotiwa kukapoteza mawasiliano na kituo cha udhibiti.

Iliarifiwa kuwa manowari hiyo ilikuwa karibu na pwani ya kaskazini ya kisiwa cha Bali kwa ajili ya zoezi la kijeshi.

Akizungumza na shirika la habari la Uingereza la Reuters, afisa mmoja wa jeshi aliripoti kwamba Australia na Singapore ziliombwa msaada kwa ajili ya shughuli ya uokoaji.

Hakuna jibu lolote lililotolewa kutoka kwa nchi hizi mbili kufuatia wito wa msaada.

Manowari ya KRI Nanggala-402, yenye uzito wa tani 1,395, ilitengenezwa nchini Ujerumani mnamo mwaka 1978 na ilikuwa imepitia kipindi cha miaka miwili ya ukarabati mnamo mwaka 2012.

Post a Comment

0 Comments