https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mbunge wa Kasulu Vijijini ampongeza Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa CCM | Muungwana BLOG

Mbunge wa Kasulu Vijijini ampongeza Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa CCM

 


Mbunge wa kasulu vijijini ndugu Vuma Augustine Holle amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samiha Suluhu Hassan kwa kuchaguliwa kwa kishindo kuwa mwenyekiti mpya wa chama cha mapinduzi (CCM).

Amesema watanzania wanatakiwa kumuunga mkono na pia rais ataendeleza yale ambayo wamefanya viongozi wengine waliopita Nyuma na anategemea mambo mengine mapya kuja kutoka kwake.

Aidha amewaomba wananchi wake wa kasulu vijijini wakae mkao wa kula Kwani kuna mazuri mengi yanakuja na akitaka kila mwananchi  kwa nafasi yake afanye kazi kwa bidii kuakikisha nchi yetu inasonga mbele maana itakuwa namna nzuri ya kumsaidia mwenyekiti mpya kutimiza ndoto.

Post a Comment

0 Comments