Papa aahidi kuizuru Lebanon, atoa wito wa kutatua mkwamo wa kisiasa


Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis, amemuahidi waziri mkuu mteule wa Lebanon Saad al-Hariri leo, kuwa ataitembelea nchi hiyo lakini baada tu ya pande za kisiasa kuweka kando tofauti zao kwa manufaa ya watu. 

Vatican imesema Hariri, ambaye pia atakutana na viongozi wa Italia wakati wa ziara yake fupi, alifanya mazungumzo na papa kwa takribani dakika 30. 

Hariri aliiambia televisheni ya Labanon baadae kwamba papa atazuru ikiwa tu wanasiasa wa taifa hilo lililogawika, wataweza kukubaliana kuhusu serikali mpya.

 Taarifa ya Vatican ilisema Francis alikariri ukaribu wake na watu wa Lebanon, wanaoishi katika nyakati ngumu na za mashaka, na kuzungumzia wajibu wa makundi yote ya kisiasa kutaguliza mbele maslahi ya taifa hilo.

Post a Comment

0 Comments