https://monetag.com/?ref_id=TTIb Uingereza yaomba msamaha kwa kushindwa kuwakumbuka wanajeshi weusi waliofarika wakati wa vita vya dunia | Muungwana BLOG

Uingereza yaomba msamaha kwa kushindwa kuwakumbuka wanajeshi weusi waliofarika wakati wa vita vya dunia


Serikali ya Uingereza imeomba msamaha kwa kufeli kuwaweka katika kumbukumbu wanajeshi weusi na wale wa kutoka bara Asia waliofariki wakipigania ufalme wa Uingereza.

Ripoti moja ya tume ya makaburi ya jumuiya ya madola ilibaini kwamba hatua hiyo ilitokana na ubaguzi.

Baadhi ya wanajeshi walikumbukwa kwa pamoja ama majina yao yalisajiliwa huku wenzao wazungu waliwekewa mawe katika makaburi yao.

Katika bunge la Uingereza waziri wa ulinzi Ben Wallace alionesha kujuta. Aliambia wabunge hakuna wasiwasi ubaguzi ulifanyika baada ya vita ya kwanza ya dunia.

Tume ya makaburi ya jumuiya ya madola pia iliomba msamaha kuhusu matokeo ya ripoti hiyo. Mbunge kutoka chama cha Leba David Lammy ambaye alikuwa kiungo muhimu katika kulianzisha suala hilo alilitaja kama 'wakati muhimu'.

Bwana Wallace alisema: Kwa niaba ya Tume ya makaburi ya jumuiya ya madola na serikali wakati huo na sasa, nataka kuomba msamaha kwa kufeli kuafikia matarajio yetu miaka yote hiyo na kuonesha kujuta kwamba imechukua muda mrefu ili kubadilisha hali hiyo. Huku tukiwa hatuwezi kubadili yaliopita, tunaweza kufanya mabadiliko na kuchukua hatua, alisema.

Uchunguzi ulianzishwa kufuatia Makala ya 2019 yaliowasilishwa na bwana lammy , kwa jina unremembered

Ulibaini kwamba takriban wanajeshi 116,000 waliofariki katika vita ya kwanza ya duniani , wengi wao wakiwa Waafrika , Wahindi ama watu waliotoka Misri , hawakukumbukwa hata kidogo''.

Pia ilibaini matamshi ya kibaguzi kama vile yale yaliotolewa na gavana mmoja wa ukoloni wa Uingereza 1923 kwamba: Watu hao wasingeweza kuelewa ama kuthamini umuhimu wa jiwe katika kaburi.."

Katika mahojiano na BBC , waziri kivuli wa haki Bwana Lammy alisema kwamba huku wakitengeneza makala hayo nchini Kenya na Tanzania , aligundua makaburi ya pamoja ambapo Waafrika walizikwa bila utambuzi wowote ule''.

Alisema kwamba ni makosa kwamba wanaume waliohudumia ufalme wa Uingereza hawakukumbukwa vyema , lakini akaunga mkono ripoti hiyo.

''Nafurahia kwamba heshima ambayo watu hawa walihitaji , baada ya kuchukuliwa kutoka katika vijiji vyao na kulazimishwa kufanyia kazi ufalme wa Uingereza na kwamba heshima waliohitaji kupewa katika kifo wanapatiwa bila kusita'', alisema.

Bwana lammy aliongezea kwamba kazi inapaswa kufanywa ili kupata majina yao katika kumbukumbu iwapo hilo litahitajika na kubaini jinsi jamii zao zinataka wakumbukwe.

Mwanahistoria Prof David Olusoga, ambaye runinga yake ilionesha unremembered, alisema kwamba tume hiyo ilijua kuhusu suala hilo na ikalazimishwa kukiri historia yake. ".

Aliambia BBC kwamba msamaha hautoshi na kwamba raslimali zitahitajika kufanya kazi iwapo tume hiyo ilikuwa tayari kulipa haki.

''Iwapo tume ya makaburi ya jumuiya ya madola iliunda kamati na kugundua kwamba wanajeshi 100,000 wa Uingereza walizikwa katika makaburi ya pamoja ambayo hayajatambuliwa na Makala hayo kuthibtisha kwamba hilo lilifanyika makusudi , je ni nini watakifanya''? aliuliza.

"Wanahitaji kupatiwa haki yao kama ile ya wale wengine na wanahitaji haki hiyo sasa hivi.

Wanajeshi wapatao milioni sita kutoka kwa ufalme wa Uingereza walihudumu katika vita ya kwanza ya dunia.

Kati ya wanajeshi 45,000 na 54,000 kutoka bara Asia na barani Afrika waliofariki katika vita hivyo walitambuliwa bila kuwepo kwa usawa, tume hiyo ilisema.

Post a Comment

0 Comments