Ujumbe wa ubaguzi uliotumwa na afisa wa polisi Ufaransa wafichuka

Imebainishwa kwamba kulikuwa na ujumbe wa kibaguzi kwenye simu ya mmoja wa maafisa wa polisi watatu ambao walituhumiwa kwa kumpiga mwanamuziki wa Kiafrika nchini Ufaransa.

Katika kipindi kimoja cha kituo cha runinga ya France 2, zilionyeshwa kanda kadhaa za simu za mmoja wa maafisa watatu wa polisi wanaotuhumiwa kwa kumpiga mwanamuziki wa Kiafrika mnamo Novemba 21 mwaka jana.

Ujumbe uliotumwa mwezi Mei katika kikundi cha mazungumzo ya polisi unaonyesha picha ya afisa wa polisi wa Marekani Derek Chauvin akimshinikiza Mwafrika-Mmarekani George Floyd shingoni mwake kwa goti. Kwenye picha, imeandikwa, "Wakati wa kuvuta hewa ya mara ya mwisho usiku kutoka kitandani."

Mnamo mwezi Agosti, polisi walituma ujumbe wa matusi kwa jamaa wa karibu wa mhathiriwa mwenye asili ya Kiafrika ambaye alikuwa akiuliza juu ya kesi hiyo. Baada ya jamaa yake kumuonya asijihusishe na ubaguzi wa rangi, polisi walidai kwamba haukuwa ubaguzi.

Katika mtaa wa 17 wa Paris, mtayarishaji wa muziki Michel Zecler alikabiliwa na vurugu za maafisa 3 wa polisi, wawili wao wakiwa wamevalia sare, ambao walikuja nyuma yake alipoingia studio yake. Baada ya wito wa msaada kutoka kwa Zecler ambaye alipigwa na polisi kwa dakika 20, majirani zake walikwenda kumsaidia kutoka kwa mlango wa nyuma wa ofisi.

Kwa kuona majirani zake, polisi walimwacha Zecler na kuondoka studio na kuita timu ya kuimarisha usalama.  Afisa wa polisi alikuwa amerusha mtungi wa gesi ya kutoa machozi ndani, na kusababisha Zecler kutoka nje.

 

Post a Comment

0 Comments