https://monetag.com/?ref_id=TTIb Waliochanjwa chanjo ya corona wazawadiwa msokoto wa bangi bure New York | Muungwana BLOG

Waliochanjwa chanjo ya corona wazawadiwa msokoto wa bangi bure New York


Wakazi wa New York jijini Marekani ambao wamekuwa wakichanjwa chanjo ya Covid-19 waliweza kupata zawadi ambayo haikutarajiwa siku ya Jumanne: Msokoto wa bangi.

Wanaharakati wanaosherehekea kuidhinishwa rasmi kwa bangi katika jimbo la New York walimpatia msokoto wa bangi wa bure mtu yeyote mjini Manhattan aliyethibitisha kuwa alipokea walau dozi moja ya chanjo moja ya corona.

"Hii ni mara ya kwanza tunaweza kuketi pamoja na kuwapatia kisheria watu bangi," alisema Michael O'Malley, mmoja wa waandalizi wa ‘’utoaji wa bangi’’ katika Union Square.

"Tunaunga mkono juhusi za shirikisho za utoaji wa chanjo. Na pia tunajaribu kuhamasisha wahalalishe kisheria matumizi ya mmea wa bangi katika nchi nzima ," aliliambia shirika la habari la AFP.

Post a Comment

0 Comments