Waturuki 16 watuzwa medali ya kifalme Uholanzi

Waturuki 16 walituzwa medali ya kifalme kwa mchango wao wa ujumuishaji kupitia shughuli za kujitolea nchini Uholanzi.

Waturuki hao waliostahili kupewa medali ya kifalme walitangazwa kuwa ni Ayşe Boya, A. Erdal, C.Sofuoğlu, G. Bozdağ-Güzel, Fatma Lapçin Yılmaz, Mevlüt Yılmaz, G. Dolu, Elif Ateş, Z. Çimtay, Fatma Kırılmaz, K. Korkmaz, N. Oral, H.İ. Seçkin, Selahattin Asal, Kerem Alan na Süreyya Erdem.

Sherehe ya utuoaji medali iliyoandaliwa katika jiji la Huizen, ilifanyika kwa kuzingatia hatua za janga.

Selahattin Asal, ambaye amekuwa akifanya kazi ya kujitolea katika msikiti wa Uholanzi kwa karibu miaka 25, alikuwa miongoni mwa waliopokea nishani ya kifalme kwenye sherehe hiyo.

Asal alipokea medali yake ya kifalme kutoka kwa meya wa Jiji la Huizen, Niek Meijer.

Tarehe ya Aprili 27, ambayo ni siku ya kuzaliwa ya Mfalme Willem Alexander, sherehe za "Siku ya Mfalme" hufanyika kote nchini Uholanzi. Watu mbalimbali kutuzwa medali ya kifalme ndani ya wiki hiyo hiyo.

Ilitangazwa kuwa medali ya kifalme, ambayo ina tahmani na umuhimu mkubwa, ilitolewa kwa watu 2,832 ikiwa ni pamoja na wanawake 998 katika miji tofauti ya Uholanzi mwaka huu.

Kufikia sasa, zaidi ya watu 150 wenye asili ya Uturuki kutoka mikoa tofauti wamepewa medali ya kifalme.

 

Post a Comment

0 Comments