Marekani yaionya Afghanistan kuhusu Taliban

Mkuu wa jeshi la Marekani, Jenerali Mark Milley amesema kuwa baada ya kuondolewa kwa askari wa Marekani kutoka Afghanistan, serikali ya Afghanistan inaweza kukabiliwa na athari mbaya kutoka kwa Taliban.

Milley amesema kwamba vikosi vya usalama vya Afghanistan vina vifaa na mafunzo mazuri, lakini hakuweza kusema kama wako tayari kwa shambulizi linaloweza kutekelezwa la Taliban bila msaada wa kimataifa.

Akiashiria kwamba kuna uwezekano pia wa upatanisho wa kisiasa kati ya serikali ya Kabul na Taliban huko Afghanistan, Milley alisisitiza kwamba ikiwa hii itatokea, vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyohofiwa vinaweza kuzuiwa.

 

Post a Comment

0 Comments