Mwanaume unapaswa kukumbuka hili katika mahusiano yako

 

Mwanaume acha ubahiri kwa sababu ni maagizo ya Mungu mwenyewe. In fact ni furaha ya mwanamke yeyote yule kuwa na mwanaume anaeweza kumhudumia mahitaji yake licha ya mwanamke nae kujikwamua kiuchumi kama ziada na nyongeza tu lakini sio wajibu wake.

Mwanaume Mungu anapokubariki na kipato sio vibaya ukamfanyia vitu vizuri mwanamke wako anataka manicure au pedicure.

Mpe fedha akaweke mwili katika mwonekano bomba! Mfanyie hata suprise ya shopping mara moja moja. Tuache ubahili, tusihonge pembeni tutafilisika, vichenchede vya nje huwa vinakamua mpaka unabaki na sharubu tu! tujifunze kuwahonga wake zetu!

Anataka vacation, peleka Ngorongoro huko huyo baby wako akashangae tembo. Anataka kula vitu vizuri, give her the treat. Kazi yako kama mwanaume ni kuhakikisha mwanamke wako anaridhika na anafurahia uwepo wako.

Kila mwanamke ni mzuri, inategemeana na wewe utakavyompa kipaumbele!

Mwanamke nae asibweteke, Mumewe anaporudi nyumbani huku akiwa na furaha ya kufanikisha dili kadhaa au huzuni ya kufeli kwa dili zake ampe mumewe maneno matamu ya kutia moyo pamoja na vitu adimu kitandani afurahie uwepo wako.

Post a Comment

0 Comments