Watu watatu wafariki kwenye shambulizi la silaha lililotokea katika duka kubwa Florida

Watu watatu walipoteza maisha katika shambulizi la silaha lililotokea kwenye duka kubwa huko Florida, USA.

Katika taarifa iliyotolewa kwenye akaunti ya Twitter ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Palm Beach, iliarifiwa kuwa shambulizi la silaha lilifanyika katika duka kubwa la Publix lililokuwa katika jiji la Royal Palm Beach.

Ilielezwa kuwa polisi waliofika katika eneo la tukio, walipata watu 3 wakiwa wamekufa ambao ni mwanamke mmoja na mtoto mmoja, katika eneo la shambulizi hilo.

Wakati hakuna taarifa iliyotolewa kuhusu chanzo cha shambulizi hilo na utambulisho wa mshukiwa, ilielezwa kuwa vikosi vya usalama vya eneo hilo vinaendeleza uchunguzi wa tukio hilo.

 

Post a Comment

0 Comments