Ethiopia yakataa kumuunga mkono bosi wa WHO kwa madai ya ‘kuunga mkono’ TPLF

 


Ethiopia ilisema jana kuwa haitaunga mkono kuchagulia tena kwa Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus wa taifa hilo kwa muhula wa pili kama mkurugenzi mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), huku ikimtuhumu kuunga mkono kundi lililopigwa marufuku.


Katika barua ya Bodi ya Utendaji ya WHO, Wizara ya Mambo ya Nje ya Ethiopia ilisema Dkt. Tedros, mwenyewe kama waziri wa zamani wa mambo ya nje, anatishia uadilifu wa shirika la WHO kwa sababu amejiunga na kundi lililopigwa marufuku katika nchi yake ya asili.


"Hajafikia uadilifu na matarajio ya kitaaluma yanayohitajika kutoka kwa afisi na wadhifa wake," ilisema barua hiyo iliyotumwa kwa Bodi, ambayo kwa sasa inaongozwa na Dkt Patrick Amoth, Daktari wa Uzazi na Magonjwa ya Wanawake na Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya ya Kenya.


"Amekuwa akiingilia masuala ya ndani ya Ethiopia, ikiwa ni pamoja na uhusiano wa Ethiopia na jimbo la Eritrea ... anaendelea kama mwanachama hai na mfuasi wa TPLF ambalo linatajwa kama kundi la kigaidi na bunge la Ethiopia.


" Ethiopia ilisema inataka Bodi, chombo chenye wanachama 34 wa WHO, kuchunguza mienendo ya Dk Tedros kwa kukiuka "wajibu wake wa kitaalamu na kisheria."

Post a Comment

0 Comments