Baraza la vyama vya siasa nchini lapongeza juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano.

Baraza la vyama vya siasa nchini limepongeza juhudi kubwa za kimaendeleo zinazofanywa na serikali ya wamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli nakusema juhudi hizo za kuleta usawa zinapaswa kuungwa mkono  na kila mtazania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa baraza hilo Mh Magalle John Shibuda, imesema inaridhishwa na kazi kubwa ina yofanywa na serikali  nakusema baraza kwa sasa linatazama namna bora ya kuboresha mazingira ya kisiasa nchini.

Aidha katika mkutano wa waandishi wa habari Dar es salaam  ulihudhuriwa na wawakilishi kutoka vyama vyote vinavyounda baraza hilo.
Mpya zaidi Nzee zaidi