Jammeh "kuachia madaraka na kuondoka"

Kiongozi wa Gambia Yahya Jammeh atawachia madaraka na kuondoka nchini Gambia, kwa mujibu wa maafisa wanaongoza mapatano.

Wapatanishi wa Afrika Magharibi watliumia masaa kadha wakikutana na bwana Jammeh siku ya Ijumaa kuzungumzia hatma yake.

Msafara wa magari uliowabeba marais wa Guinea na Mauritania, umeondoka makao ya Jammeh lakini hayaaminiwi kuondoka nchi humo.

Bwana Jammeh alishindwa kwenye uchaguzi wa mwezi Disemba na mrithi wake Adama Barrow ameapishwa.

Jammeh alikuwa amepewa makataa ya kuondoka madarakani kufikia saa sita mchana la sivyo aondolewe kwa nguvu na wanajeshi wanaoungwa mkono na UMoja wa Mataifa.


JIUNGE NASI KATIKA
INSTAGRAM @Muungwanablog

FACEBOOK @Muungwana Blog

YOUTUBE @Muungwana Tube

BOFYA HAPA KU-INSTALLAPP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.