Jinsi ya kupika Shurba chukuchuku

Kutokana na familia yangu kuepuka sana Kula Mafuta hivyo vyakula vyetu vingi ninaepuka kutumia mafuta mengi wakati wa kupika au kutoweka Kabisa.

Hivyo nimeamua kutwist recipe ya  Shruba nimeamua kufanya chukuchuku.
Usijali  nitaweka inayotumia mafuta.

Mahitaji 

  1. Oats / ngano  nusu kikombe
  2. Nyama (mbavu) nusu kilo
  3. Nyanya fresh moja
  4. Kitunguu maji kimoja kikubwa
  5. Kitunguu swaumu kijiko cha chakula1
  6. Pilipili manga kijiko cha chai 1
  7. Chumvi nusu kijiko cha chai
  8. Viungo vya pilau  kijiko cha chakula1
  9. Unga wa ngano kijiko kimoja cha chakula
  10. Korianda


Jinsi ya Kupika

  • Chemsha oats/ngano  weka pembeni
  • Osha nyama yako weka katika sufuria chemsha ikiiva iache na supu
  • Saga viungo vyote pamoja weka 
  • mimina katika nyama,weka viungo vya pilau,mag,pilipili manga,wacha vichemke kwa pamoja kwa dakika tano halafu weka ngano funika wacha ichemke wa nusu saa. 
  • Weka unga wa ngano katika kibakuli n.a. maji mimina katika shruba  wacha uchemke kwa dakika 10. 


Epua tayari kwa kuliwa..
NB:Wakati wa kunywa waweza weka siki au ndimu upendavyo



JIUNGE NASI 

 INSTA@MUUNGWANABLOG ,FB@MUUNGWANABLOG,YOUTUBE @MUUNGWANA TUBE, BOFYA HAPA KU-INSTALL APP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.

Mpya zaidi Nzee zaidi