News alert: moto wazuka katika uwanja wa klabu ya Manchester United Old Trafford





  Sehemu ya uwanja wa klabu ya Manchester United Old Trafford ulishika moto asubuhi ya leo kabla vikosi vya zimamoto kufika na kuuzima.

Shuhuda wanasema walianza kuona moshi mkubwa ukifuka  katika jukwaa la kusini la uwanja huo maarufu liitwalo Sir Bobby Sharlton Stand.Klabu ya Manchester united ilisema katika twitter yake kuwa moto mdogo uliosababishwa na hitilafu ya umeme ulizuka kwenye moja ya lifti na wazima moto waliitwa na kufanikiwa kuuzima. Hakuna madhara makubwa yaliyotokea.

  Vikosi vya zimamoto vikiwa vimeudhibiti moto huo
Jukwaa ulikozukia moto huo

Mpya zaidi Nzee zaidi