Wakisaini Mkataba katikati ni Mstahiki Meya Wa Manispaa ya Ilala Bw Abadallah Chaulembo,Kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Bw Nassib Mbaga na Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Ujenzi CRJE Bw Zhao Yefang
Katibu mkuu wa Wilaya ya Temeke Bw Hashim Komba akiongea na Wananchi wa Kijichi kuhusu swala zima la Utengenezwaji wa Daraja hilo ili kuondoa Usumbufu wanaoupata wananchi kuzunguka Kigamboni na Kongowe wakati wa Msimu wa Masika.
Mstahiki Meya wa Temeke Bw Abdallah Chaulembo akizungumza na wananchi wa Kijichi kuhusu ujenzi wa Daraja unaotarajia kuanza mapema Mwaka huu katika Eneo hilo
Baadhi ya Wananchi wa Kijichi wakiwa Katika Mkutano huo.
Serikali ya Manispaa ya wilaya ya Temekee na kampuni ya Ujenzi ya China CRJE wametiliana saini mkataba wa Ujenzi wa Daraja litakalo unganisha eneo la kijichi na Tuangoma wilayani humo.
Akizungumza katika hafla hiyo mwakilishi wa Mkuu wa wilaya ya Temeke ambaye pia ni katibu tawala Wilaya hiyo Hashim Komba , amesema daraja hilo linajengwa ili kuondo usumbufu wanaoupata wananchi wanaoishi maeneo hayo kwa kuzunguka Kigamboni na kongowe wakati wa masika.
Aidha afafanua kuwa Daraja hilo litakuwa na urefu wa Mita 800 na barabara za mitaa zaidi ya kumi zenye urefu wa Kilomita 1.8 na barabara nyingine zenye urefu wa kilomita 84 zote zitajengwa kwa kiwango cha lami na kitapimwa viwanja zaidi ya mianane kuzunguka eneo la mradi huo.
Naye Mkurugenzi wa kampuni ya Ujenzi CRJE Zhao Yefang ameshukuru kupewa kazi hiyo ana ameahidi kufanya kwa viwango kama walivyo jenga Daraja la Kigamboni watahakikisha ubora na thamani ya hela vinazingatiwa na ndani ya mwaka mmoja watakabidhi Daraja hilo.
Katibu mkuu wa Wilaya ya Temeke Bw Hashim Komba akiongea na Wananchi wa Kijichi kuhusu swala zima la Utengenezwaji wa Daraja hilo ili kuondoa Usumbufu wanaoupata wananchi kuzunguka Kigamboni na Kongowe wakati wa Msimu wa Masika.
Mstahiki Meya wa Temeke Bw Abdallah Chaulembo akizungumza na wananchi wa Kijichi kuhusu ujenzi wa Daraja unaotarajia kuanza mapema Mwaka huu katika Eneo hilo
Baadhi ya Wananchi wa Kijichi wakiwa Katika Mkutano huo.
Serikali ya Manispaa ya wilaya ya Temekee na kampuni ya Ujenzi ya China CRJE wametiliana saini mkataba wa Ujenzi wa Daraja litakalo unganisha eneo la kijichi na Tuangoma wilayani humo.
Akizungumza katika hafla hiyo mwakilishi wa Mkuu wa wilaya ya Temeke ambaye pia ni katibu tawala Wilaya hiyo Hashim Komba , amesema daraja hilo linajengwa ili kuondo usumbufu wanaoupata wananchi wanaoishi maeneo hayo kwa kuzunguka Kigamboni na kongowe wakati wa masika.
Aidha afafanua kuwa Daraja hilo litakuwa na urefu wa Mita 800 na barabara za mitaa zaidi ya kumi zenye urefu wa Kilomita 1.8 na barabara nyingine zenye urefu wa kilomita 84 zote zitajengwa kwa kiwango cha lami na kitapimwa viwanja zaidi ya mianane kuzunguka eneo la mradi huo.
Naye Mkurugenzi wa kampuni ya Ujenzi CRJE Zhao Yefang ameshukuru kupewa kazi hiyo ana ameahidi kufanya kwa viwango kama walivyo jenga Daraja la Kigamboni watahakikisha ubora na thamani ya hela vinazingatiwa na ndani ya mwaka mmoja watakabidhi Daraja hilo.
JIUNGE NASI KATIKA
INSTAGRAM @Muungwanablog
FACEBOOK @Muungwana Blog
YOUTUBE @Muungwana Tube
BOFYA HAPA KU-INSTALLAPP YA MUUNGWANA BLOG ILI UPATE URAHISI KUZISOMA HABARI ZOTE KWA WAKATI.



