Wasanii Wa Tanzania Wafanya Maonyesho Nairobi

 Wasanii wachoraji 14 kutoka Tanzania wamewasili Nairobi kufanya maonyesho ya kazi zao katika tamasha la majuma mawili kwenye ukumbi wa Village Market litakaloanza rasmi Jumatano tarehe 25 Januari. Kundi hilo lilitembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya leo na kukutana na Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed Waziri.

Msemaji wa Kundi hilo, Bw. Amani Abeid, alisema lengo lao ni kutambulisha kazi zao katika soko la Kenya na kuwa baada ya hapo wataelekea Rwanda. Washiriki kwenye maonyesho hayo ya Nairobi ni Cathbert Semgoja, Masoud Kibwana, Haji Chilonga, Amani Abeid, Localfanatics, Nadir Tharan, Thobias Minzi, Lutengano Mwakisopile, Moses Luhanga, Raza Mohammed, Ludovic Kaija, Cloud Chatanda na Salum Kambi.

Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Bi. Talha Mohamed Waziri (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wasanii kutoka Tanzania ambao wako jijini Nairobi kufanya Maonyesho ya Sanaa Oni.
Mpya zaidi Nzee zaidi