Familia yaisoma namba kwa mkataba wa Q Chillah

Q Chillah

 Familia ya msanii wa bongo fleva Q Chilla wameamua kuingilia kati mkataba wa msanii huyo na kusema mkataba huo unamfanya aishi maisha magumu kiasi cha kushindwa kuchangia mambo yakifamilia.

Akiongea kupitia eNewz ya EATV, baba mdogo wa Q Chila amesema kwamba hofu juu ya mkataba ni kwamba haukuwa na ushahidi wowote kwa upande wa Q Chilla hali inayombana na kushindwa kuendelea kimaisha na kushindwa kuwa na  nyumba yake.

Amesema familia hiyo imeamua kumuandikia barua bosi wa Q Chillah ambaye ni QS Mhonda kumuomba kubadilisha sehemu mbalimbali ambazo zinambana sana kijana wao kiasi cha kumsababishia kurudi alipotoka jambo linaloweza kumvurugia maisha yake.
Tazama hapa alipokuwa akizungumza na eNewz

VIDEO: Huyu jamaa ana kipaji cha kula


Mpya zaidi Nzee zaidi