Manji Awarudisha Kundini Hashim, Mkemi Na Nyenzi

 UONGOZI wa Yanga SC, umewasamehe na kuwarejesha kundini wanachama wake watatu, Ayoub Nyenzi, Hashim Abdallah na Salum Mkemi ambao walisimamishwa katika Mkutano wa Agosti 6, mwaka jana.

Taarifa ya Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa kwa vyombo vya Habari leo imesema kwamba Mwenyekiti wa klabu, Yussuf Manji ametoa msamaha kwa wanachama hao, ambao pia walikuwa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji.

Katika mkutano Mkuu wa dharula wa Yanga SC Agosti 6, mwaka jana, Manji mwenyewe aliwafukuza uanachama Mkemi, Abdallah na Nyenzi kwa sababu alisema hayuko tayari kufanya kazi na Wajumbe hao wa Kamati ya Utendaji.








VIDEO; CHEKA NA MLOKOLE

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items