Madhabahu hayo ni miongoni mwa madhabahu matakatifu zaidi Pakistan
Mshambuliaji wa kujitoa mhanga alijilipua katika katikati mwa waumini katika madhabahu ya Wasufi ya mtakatifu Lal Shahbaz Qalandar katika mji wa Sehwan, mkoa wa Sindh.
Waziri mkuu Nawaz Sharif amelaani shambulio hilo.
Wapiganaji wa Islamic State, Taliban nchini Pakistan na makundi mengine ya wanamgambo, wamekiri kuhusika.
Madhabahu hayo ni miongoni mwa yale ya kale zaidi na yanayotukuzwa sana na yalikuwa yamejaa watu Alhamisi, kwani siku hiyo huchukuliwa kuwa tukufu kwa Waislamu kufanya sala katika madhabahu hayo.
Walioshuhudia wanasema mshambuliaji alijilipua watu walipokuwa wakicheza dansi ya imani.
Vyombo vya habari zinasema alirusha guruneti nakisha akajilipua.
"Niliona miili imetapakaa kote. Niliiona miili ya wanawake na watoto," mwanamume mmoja aliwaambia wanahabari.
Mshambuliaji alijilipua watu waliokuwa wakicheza dansi takatifu
Watoto ni miongoni mwa waliojeruhiwa



