CUF Wadai Kuwepo Mpango wa Kumuhujumu Maalim Seif


Chama cha Wananchi (CUF) kimedai kuna mipango inayofanyika ya kumvua ukatibu mkuu Maalim Seif Sharif Hamad kwa sababu anaonekana kama kikwazo cha utulivu Zanzibar.

Katika taarifa iliyotolewa na chama hicho jana, ilidai kuna kikao cha chini chini ambacho kimeandaliwa na baadhi ya wajumbe wa upande mmoja wa CUF, kikiwa na lengo hilo huku upande wa pili ikipinga kikao hicho ambacho hakitambuliki kikatiba.

“Kwa mujibu wa katiba ya CUF Ibara ya 84 (1) ikisomwa pamoja na ibara ya 93 (1)(d) inaeleza kuwa; ...kutakuwa na Kamati ya Utendaji ya Taifa ambayo itakutana mara moja kwa kila miezi miwili,” ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ilitolewa jana na Katibu Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma, Mbarara Maharagande ilieleza mara ya mwisho kikao cha kawaida cha Kamati ya Utendaji ya Taifa kilifanyika Februari 2, 2017 katika ofisi ndogo ya chama Vuga, Mjini Unguja.






Umeshawahi Kufikiria Kupata Gari la Bure bila Kulipa Chochote, Basi hii Kampuni ya Cars From Japan Wanakupa Nafasi Hiyo ... 

Chakufanya ni Kubofya Link hapo chini na Ufate Maelekezo ya Jinsi ya Kuweza Kuwa Mshindi wa Gari hilo..

Kisha Jisajili kwa Kuweka Jina na Email Yako... USIWE NA WASIWASI HUDUMA HII NI SALAMA KABISA..

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Ujuwe Ugonjwa wa Busha

Kilimo cha Bamia