Jeshi la polisi Zanzibar lathibitisha maofisa wake watano kutuhumiwa kuhusika usambazaji wa dawa za kulevya.

Jeshi la polisi Zanzibar limethibitisha kwa maofisa wake watano wanatuhumiwa kuhusika na uletaji,uingizaji na usambazaji wa madawa ya kulevya na tayari maofisa hao wanashugulikwa katika ngazi za juu la jeshi hilo nchini.

Kauli hiyo imetolewa na  mkuu wa jeshi la polisi  Kamisheni ya  Zanzibar Kamishna Mkuu CP Hamdan Omar Makame wakati akizungumza na maofisa na askari wa mikoa mitatu ya Unguja kuelezea  hali ya operesheni ya vita ya dawa za kulevya na udhalilshaji wa wanawake na watoto ambapo amesema Polisi ndio wanatakiwa kuwa wasimamzi wa sheria na kuwa mstari wa mbele  hivyo jambo hilo halikubaliki  na taratibu za kisheria zimeshanza dhidi ya maofisa hao watano wanotuhumiwa kuhusika kwa njia zote.

CP Hamdan Omar Makame ambaye amewanyoshea kidole askari ambao wanazipinda sheria kwa makusudi wakati wanapoona uhalifu umefanyika  waache na sheria ifuatwe na watakaobainika watatimuliwa kwa mujibu wa sheria huku akitangaza kuanza rasmi  oparesheni maalum inayowashirikisha  jeshi la polisi,afisi za waendesha mashataka na  mahakama kuu  katika kupambana na vitendo vya udhalilishaji na tayari mahakimu na majaji wameshateuliwa kusimamia kesi hizo kuanzia leo na wanatarijia kuwepo na kuanza  kwa kesi 25.

Hatua hizo za jeshi la polisi ambazo zinapaswa kuungwa mkono na jamii zinakuja huku pakiwemo na msukumo mkubwa wa serikali kutaka polisi na vyombo vya ulinzi na usalama kuhakiksiha kwa nguvu zote wanakomesha vita dhidi ya dawa za kulevya na udhalilishaji  Kisiwani  Zanzibar.
Mpya zaidi Nzee zaidi