Leo April 19, Umoja wa Wasanii wa Bongo Movie Kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam chini ya Paul Makonda Wamefanya maandamano ya amani kutoka Katika ofisi ya Mkuu ya Mkoa kuelekea Eneo la kariakoo, kwa lengo la kufanya mkutano wa kuzuia Uingizwaji na Uuzwaji wa filamu kutoka Nje ya nchi kinyume cha utaratibu.
Mara baada ya kuwasili eneo la Kariakoo, Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amewataja watu 13 ambao wanahitajika kujipeleka katika kituo cha kati cha Polisi Jijini humo siku ya ijumaa kwa ajili ya kuhojiwa kuhusiana na matumizi ya mitambo ya kzalishia filamu. Pamoja na kuzuia filamu za ngono zisiingie mkoa wa Dar es salaam na wasipojipeleka atawafuta mwenyewe.
Baadhi ya Wasanii waliohudhuria ni Wolper, JB, Kajala, Ray Kigosi, Richi Richi, Radio na Mafuvu.
TAZAMA VIDEO NZIMA HAPO CHINI...
