Safaricom yakumbwa na matatizo ya mawasiliano Kenya

 Hitilafu imeathiri pia M-Pesa inayotumiwa na zaidi ya watu 20 milioni

Kampuni kubwa ya mawasiliano nchini Kenya Safaricom imekumbwa na matatizo ya kiufundi ambayo yameathiri huduma zake za simu.

Safaricom imesema hitilafu hiyo imeathiri huduma zake kote nchini.

"Tunakabiliwa na tatizo la kuunganisha simu, data na huduma ya M-Pesa. Tatizo hili kwa sasa linaangaziwa. Samahani kwa usumbufu," kampuni hiyo imeambiwa wateja kupitia Twitter.

Jina la kampuni hiyo limeanza kuvuma katika mitandao ya kijamii, wateja wakitaka kujua nini sababu yao kushindwa kupiga simu na kupokea au kutuma pesa.
Majibu ya Safaricom kwa wateja waliokuwa wakilalamikia kampuni hiyo kwenye Twitter
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Ujuwe Ugonjwa wa Busha

Kilimo cha Bamia