Mbunge wa Jimbo la Kinondoni amdhamini Bondia Amosi Mwamakula anayetarajia kupeperusha Bendera ya Tanzania kwenye pambano lake na Bondia kutoka Nchini Malawi.
Super Kyela atapambana na Odesen Kayuni kutoka Malawi.
Mbunge Mtulia amesema kuwa atadhamini pambano hilo la Kimataifa litakalo fanyika tarehe 8 Agosti Mwaka Kwenye Ukumbi wa Traval Train ilikuwepo Magomeni Mikumi Dar es Salaam.
Pambano hilo litasindikizwa na Bondia Nguli Francis Miyeyusho,Ibrahimu Tampa, Ibrahimu Class Haidari Mchanjo, Iddi Mkwera, Vicent Mbilinyi na Mabonde wengine kutoka Nje na ndani ya Nchi.
kwa upande wake Super Kelya amempongeza Mbunge huyo kwa mchango huo kwenye pambano lake na kwamba ni sehemu ya kukuza vipaji vya mchezo huo kama alivyo ahidi kwenye kampeni zake za 2015.

