Cervical Cancer Saratani Ya Mlango Wa Kizazi

Saratani ya mlango wa kizazi 
Hii ni njia ya kizazi kati ya uke na mji wa mamba.Ugonjwa huu ukijulikana mapema unweza kutibiwa, wakati wa kufanyiwa uchunguzi wa ubwabwa na fupa nyongo.

Nani yumo hatarini
Wanawake wengine wamo hatarini mwa kupata saratani ya mlango wa kizazi:
Wanawake wasioenda kwa uchunguzi wa kila mwaka wa fupa nyongo na ubwabwa
Wanawake walio na “human papillomavirus” HPV au genital warts
Kuvuta sigara, kuwa na ukimwi,na kutokula vyakula bora huweza kusababisha saratani ya mlango wa kizazi.

Dalili ya saratani ya mlango wa kizazi
Hamna dalili zozote mpaka unaposambaa nje ya mlango wa kizazi.

Hali hii ikitokea waweza kuwa:

  • Kuvuja damu katikati ya siku za hedhi, unaposhiriki ngono au baada ya hedhi kukatika
  • Kuvuja damu nyingi zaidi ya kawaida.
  • Ukiona dalili hizi pata ushauri wa daktari.


Saratani ya Utumbo Mpana na Sehemu za Siri za Nyuma 
Saratani ya sehemu za siri za nyuma zipo. Huambukiza sehemu za mmeng’enyo (digestive system) wa chakula. Watu wengi wanaopata ugonjwa huu ni wa umri wa zaidi ya miaka 50.

Matibabu yake yameimarika, lakini ni vyema kugundua mapema.Watu wanahitaji kufahamu madhara, dalili na umuhimu wa kupimwa na madaktari wao.

Walio hatarini kupatwa na saratani ya utumbo mpana:
  • Ajuza wa miaka 50 na zaidi.
  • Wanaokula vyakula vya mafuta mengi
  • Walio na maoteo (ndani ya utumbo mpana )
  • Wanawake ambao washaugua saratani ya matiti, au mji wa mimba au yai la mwanamke
  • Aliye wahi kuugua saratani ya utumbo mpana
  • Aliye na mzazi, jamaa au motto aliye na saratani ya utumbo mpana
  • Aliye na utumbo mpana wenye kiungulia (donda au uvimbe)


Dalili za saratani ya utumbo mpana ni:
  • Kuvimbiwa, kusokotwa au kujihisi tumbo limejaa sehemu ya chini
  • Kuhara, kufunga choo au kujihisi haukamilishi haja kabisa
  • Damu katika kinyesi
  • Kinyesi chembamba zaidi
  • Kupoteza uzito bila ya kufahamu kisababu
  • Kujihisi mchovu kila wakati
  • Kutapika
  • Hizi dalili zinaweza kusababishwa na shida nyingine ambazo si saratani. Muulize daktari wako ili ufahamu

Saratani ya Mapafu 
Saratani ya mapafu ndio aina hatari ya magonjwa ya saratani, lakini ndio rahisi kuzuia.Uvutaji wa sigara husababisha asilimia 9% kwa 10% ya kesi za ugonjwa huu.Matibabu ya ugonjwa huu yameimarika lakini bado hakuna tiba.Ili kuimarisha afya yako na walio karibu yako usivute sigara.
Pia hakikisha nyumba yako haina 'radon' gesi hatari isababishayo saratani ya mapafu.

Watu wengine wamo hatarini zaidi ya kupata saratani ya mapafu.
Wanaovuta sigara au kiko, na hata usipo vuta moshi ndani, umo hatarini kupata saratani ya domo. Kukaa karibu na mvutaji sigara au kuishi naye ama kufanya kazi katika mazingira yenye moshi huongeza hatari hasa kwa watoto wasio na namna.
Kiwango kingi cha madini ya radon nyumbani mwako.
Kufanya kazi karibu na asbestos, aseniki, uranium au bidhaa kutokana na mafuta.
Kuwa na kifua kikuu.

Ishara ya saratani ya mapafu ni nini? 
  • Kikohozi kisicho kwisha.
  • Kuumwa na kifua.
  • Kukohoa damu
  • Shida ya kupumua au kukorota upumuapo
  • Nimonia(kichomi) au mkamba usiyokwisha
  • Uvimbe shingoni au usoni.
  • Kupoteza uzito wako bila sababu au kutohisi njaa.
  • Kujihisi mchovi kila wakati.


Ukiwa na mojawapo ya dalili hizi, hasa ikiwa umo hatarini ya kupata huu ugonjwa, mwone daktari.


Saratani ya Mdomo 
Saratani ya mdomo husambaa kinywani kwenye ulimi, ufizi, kidakatonge na koromeo.Watu hawatambui ugonjwa huu upesi.Wanaovuta sigara,kuvuta tumbako au kunywa kunywa pombe wamo hatarini mwa kupata sratani yam domo.Unaweza kusaidiwa ili kuwacha sigara au pombe.Ugonjwa huu unaweza kitibiwa ukiuwahi mapema.


Ishara ya saratani ya Mdomo ni kama zifuatazo;

  • Uvimbe sehemu yoyote mdomoni, ambao hauponiau kutokuwa na damu kwa urahisi.
  • Kuhisi uchungu au kufa ganzi mdomoni.
  • Kuhisi uchungu unapo tafuna, kumeza chakula ulimi unapotumika au taya.
  • Kubadilika kwa sauti yako.
  • Kuumwa na sikio.
  • Koo linalowasha bila kupona.
  • Ukiwa na ishara hizi mwone daktari haraka sana.