Beki wa kulia wa timu ya Simba, Shomari Kapombe atalazimika kubakia Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu kufuatia majeraha ya kuvunjika mguu aliyoyapata akiwa na timu ya taifa,Taifa Stars nchini Afrika Kusini.
Kapombe aliumia akiwa kwenye kambi ya timu ya Taifa iliyokuwa inajiaanda na kucheza mchezo wa kufuzu Afcon uliopigwa kwenye uwanja wa Setsoto Maseru nchini Lesotho jana na inaelezwa kuwa atakaa nje kwa muda wa miezi mitatu.
Taarifa kutoka ndani ya Simba zimeeleza kuwa beki huyo atalazimika kubakia Afrika Kusini kwa ajli ya kupatiwa matibabu kwa daktari wake maalum kabla ya kurejea nchini kuendelea na majukumu ya timu yake.
Awali uongozi wa shirikisho la soka la Tanzania (TFF) ulipanga kumpeleka nchini Dubai kwa ajili ya kupata matibabu hayo lakini uongozi wa Simba ukapendekeza abakie Afrika Kusini kwa kuwa ana daktari wake maalum.
Kapombe amevunjika mguu karibu na eneo la enka hali ambayo ilisababisha akose mchezo wa jana ambao ulimalzika kwa Stars kufungwa bao 1-0.
Kapombe aliumia akiwa kwenye kambi ya timu ya Taifa iliyokuwa inajiaanda na kucheza mchezo wa kufuzu Afcon uliopigwa kwenye uwanja wa Setsoto Maseru nchini Lesotho jana na inaelezwa kuwa atakaa nje kwa muda wa miezi mitatu.
Taarifa kutoka ndani ya Simba zimeeleza kuwa beki huyo atalazimika kubakia Afrika Kusini kwa ajli ya kupatiwa matibabu kwa daktari wake maalum kabla ya kurejea nchini kuendelea na majukumu ya timu yake.
Awali uongozi wa shirikisho la soka la Tanzania (TFF) ulipanga kumpeleka nchini Dubai kwa ajili ya kupata matibabu hayo lakini uongozi wa Simba ukapendekeza abakie Afrika Kusini kwa kuwa ana daktari wake maalum.
Kapombe amevunjika mguu karibu na eneo la enka hali ambayo ilisababisha akose mchezo wa jana ambao ulimalzika kwa Stars kufungwa bao 1-0.
