Rais Kim aishutumu Marekani kwa 'kupotosha ukweli' kuhusu mpango wa nyuklia


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ameishutumu marekani kwa "kupotosha ukweli" wakati wa mkutano mapema wiki hii na rais Donald Trump, kwa mujibu wa shirika la habari la Korea -Korea Central News Agency.

Amesema pia kwamba amani katika rasi ya Korea itategemea utawala wa Washington, Bwana Kim aliitoa kauli yake katika mkutano wa Alhamisi na rais wa Urusi Vladimir Putin katika mji wa Vladivostok.

Rais Putin alikubali mwaliko wa kuizuru Korea Kaskazini, KCNA limeripoti, Ziara hiyo itafanyika "katika wakati unaofaa ," shirika hilo la habari limeongeza kusema.

Kim Jong-un anaripotiwa kumwambia Vladimir Putin kwamba "hali katika rasi ya Korea peninsula na kanda hiyo kwa ujumla tete na imefikia wakati mgumu".

Alionya kuwa hali "inaweza kurejea mahali ilipokuwa kwasababu Marekani imeamua kuchukua mkondo wa ''kupotosha ukweli " wakati wa mazungumzo ya hivi karibuni.

Hii inakuja wiki moja baada ya Pyongyang kuishutumu Marekani kuvuruga mazungumzo ya amani,
Mazungumzo baina ya nchi mbili yalivujika wakati wa kikao cha Vietnam mwezi Februari, bila kufikiwa kwa mkataba juu ya silaha za nuklia za Korea kaskazini .