BREAKING: Zaidi ya watu 60 wanasadikiwa kuungua moto


Zaidi ya watu 60 wanasadikiwa kuungua moto na kupoteza maisha baada ya gari la mafuta kulipuka na kuwaka moto Msamvu Itigi mkoani Morogoro.

Tukio hilo limetokea leo Jumamosi ambapo miili iliyoungua ikiwa imelazwa pembeni ya barabara ya  Dar es Salaam-Morogoro wengi wakiwa ni madereva bodaboda na mamalishe wanaofanya shughuli zao hapo.

Idadi ya vifo mpaka sasa ni 60 na majeruhi ni 70.

Endelea kufuatilia Muungwana Blog kwa taarifa zaidi.