Kifo cha msanii huyo mkongwe kimethibitishwa na mtoto wake wa kiume, Adam Juma, ambaye amesema kuwa mama yake alikuwa akisumbuliwa na tatizo la moyo.
Familia ya marehemu inaendelea na mipango ya mazishi ambayo itaitangaza.
Bi Cheka atakumbukwa kwa umahiri wake wa ku-rap ambapo aliwahi kufanya kazi nyingi za muziki hasa akiwa na Kundi la TMK. Baadhi ya wasanii aliowahi kufanya nao ngoma ni Mheshimiwa Temba na marehemu Godzilla.